Sunday, December 30, 2012

Saturday, December 29, 2012

Friday, December 28, 2012

Ukweli Kuhusu Lamborghini ya Video ya Naija Girl ya Prezzo

Baada Ya Stori na picha Kusambaa ikimuonesha Prezzo akiwa na Gari la kifahari aina ya Lamborghini Team nzima ya RICHARD KADURI.blogspot.com Tuliona si mbaya Tukatafuta ukweli kuhusu Prezzo na his new Ride..
Gari hilo si la PREZZZO bali mliki halisi ni Msanii toka pande za Nigeria anayetamba na wimbo wa Skibobo alioshirikishwa mkali wa Bongo AY'(Goldie)

Bwana mkubwa ameazima mkoko huo kwa ajili ya Kushoot video ya wimbo wake wa Naija Girl...

Watu walianza kuhesabu thamani ya mali ya Prezzo kumbe Goldie ni zaidi yake..

Thursday, December 27, 2012

Wednesday, December 26, 2012

Monday, December 24, 2012

Sunday, December 23, 2012

Saturday, December 22, 2012

Friday, December 21, 2012

Wednesday, December 19, 2012

Sunday, December 16, 2012

Monday, December 10, 2012

Ray C Amshukuru Rais Kikwete kwa Msaada wa Matibabu

Msanii wa Kizazi Kipya Rehema Chalamila 'Ray C'  Akiwa ameambatana  na Mama yake Mzazi Magreth Mtweve na Dada yake Sara Mtweve wamemshukuru Rais Kikwete kwa msaada wa Matibabu na Kumueleza  Kuwa afya ya Mwanae imeimarika na Muda c mrefu ataendelea kupanda jukwaani.
Mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya, Rehema Chalamila 'RAY C' akimshukuru Rais Kikwete kwa msaada wa matibabu aliompatia ikulu jijini Dar es Salaam leo.

Cortez Bryant Meneja wa Nicki Minaj Aziponda Nomination za Tuzo za Grammy

Cortez Bryant meneja wa Nicki Minaj ameziponda nomination za Tuzo za Grammy zilizotajwa siku kadhaa zilizopita ikiwa ni siku chache baada ya Meneja wa Justine Bieber Scooter Braun Kuziponda tuzo hizo kwa madai yanayofanana na ya Bryant

 Nicki Minaj pamoja na kutoa Album yake mpya hivi karibuni “Pink Friday: Roman Reloaded.” na Bieber nae kutoka na Albaum na tour yake iliyobamba zaidi 'Believe' na kuonekana kuvutia wengi lakini hawakutajwa kuwania hata category moja mwaka 2013 katika  nomination hizo.




 Cortez Bryant ambaye pia ni meneja wa Young Money Lil Wayne, Drake na Nicki Minaj aliposti katika mtandao wa kijamii wa twitter kwa kuziita "Bulls***" na alianza kwa hongera lakini akaponda utaratibu wa tuzo hizo  “Congrats to @LilTunechi and@Drake and@Hit Boy on their Grammy Noms butt....,
 Drake na Lilly Weezy wamekuwa nominated katika collabo yao ya HYFR na The Motto pia Drake binafsi amekuwa nominated kwenye category ya Best Rap Album.

Meneja  wa Biebs alitweet, "The hardest thing to do is transition, keep the train moving. the kid delivered. Huge succesful album, sold out tour, and won people over."










Nicki Minaj alikuwa nominated mara tatu katika tuzo hizo mwaka jana lakini lakini hakupata nafasi ya kuchukua tuzo hata moja. Kwa mwaka huu majina makubwa kama Lady Gaga na mwanamuziki kutoka Korea PSY mzee wa ‘Gangnam Style’ ambao watu wengi walitarajia kuonekana katika tuzo lakini hali imekuwa tofauti.      

Friday, December 7, 2012

Jay-Z, Kanye West, Frank Ocean, Black Keys waongoza Nomination list tuzo za Grammy 2013

Wasanii wa muziki wanowania za ‘Grammy awards 2013’ tuzo ambazo ni maarufu na zenye heshima kubwa Duniani, wametangazwa rasmi jumatano ya tarehe 5, December, Brindgestone Arena huko Nashville, Tennessee.




Katika nomination hizo  makundi ya muziki kadhaa na wanamuziki waliopata nafasi ya kutajwa kushindania tuzo katika cartegory zaidi ya moja ni; Jay- Z, Kanye West, Frank Ocean, Fun, na The Black Keys, Mumfrod &Sons.

K The Black Keys ni kundi la muziki wa Rock lililochaguliwa katika Cartegory tano wakati member wa kundi hilo Dan Aurbach akipata akitajwa kushindania category moja ‘non-classical producer of the year’.  The Black Keys wametajwa katika category ya Album of the Year and Best Rock Album “El Camino”, na Record of the Year, Best Rock Performance na Best Rock Song kwa wimbo wao “Loney Boy”.

Category sita zimetajwa kushindaniwa na Jay-Z na Kanye West na majina yao yaling'ara kwa sababu ya album yao ‘Watch the Throne’ waliofanya pamoja na baadhi ya kazi zao walizofanya individually.

Hizi ni tuzo za 55 za Grammy tangu zianze kutolewa na zinatarajiwa kufanyika February 10, 2013 saa mbili usiku kwa saa za Afrika Mashariki, Kutoka Staples Center, Los Angeles.

Baadhi ya nomination list ya tuzo hizi za Grammy 2013.

Album Of The Year:
•             "El Camino" - The Black Keys
•             "Some Nights" - Fun.
•             "Babel" - Mumford & Sons
•             "Channel Orange" - Frank Ocean
•             "Blunderbuss" - Jack White

Record Of The Year:
•             "Lonely Boy" - The Black Keys
•             "Stronger (What Doesn't Kill You)" - Kelly Clarkson
•             "We Are Young" - Fun. featuring Janelle Monae
•             "Somebody That I Used To Know" - Gotye featuring Kimbra
•             "Thinkin Bout You" - Frank Ocean
•             "We Are Never Ever Getting Back Together" - Taylor Swift

Best New Artist:
•             Alabama Shakes
•             Fun.
•             Hunter Hayes
•             The Lumineers
•             Frank Ocean

Song Of The Year:
•             "The A Team" - Ed Sheeran
•             "Adorn" - Miguel
•             "Call Me Maybe" - Carly Rae Jepsen
•             "Stronger (What Doesn't Kill You)" - Kelly Clarkson
•             "We Are Young" - Fun.

Best Pop Solo Performance:
•             "Set Fire to the Rain (Live)" - Adele
•             "Stronger (What Doesn't Kill You)" - Kelly Clarkson
•             "Call Me Maybe" - Carly Rae Jepsen
•             "Wide Awake" - Katy Perry
•             "Where Have You Been" - Rihanna

Best Rock Album:
•             "El Camino" - The Black Keys
•             "Mylo Xyloto" - Coldplay
•             "The 2nd Law" - Muse
•             "Wrecking Ball" - Bruce Springsteen
•             "Blunderbuss" - Jack White

Best Rock Song:
•             "Freedom at 21" - Jack White
•             "I Will Wait" - Mumford & Sons
•             "Lonely Boy" - The Black Keys
•             "Madness" - Muse
•             "We Take Care of Our Own" - Bruce Springsteen

Best R&B Album:
•             "Black Radio" - Robert Glasper Experiment
•             "Back to Love" - Anthony Hamilton
•             "Write Me Back" - R. Kelly
•             "Beautiful Surprise" - Tamia
•             "Open Invitation" - Tyrese Gibson

Best R&B Song:
•             "Adorn" - Miguel
•             "Beautiful Surprise" - Tamia
•             "Heart Attack" - Trey Songz
•             "Pray for Me" - Anthony Hamilton
•             "Refill" - Elle Varner

Best Rap Album:
•             "Take Care" - Drake
•             "Food and Liquor 2: The Great American Rap Album Pt. 1" - Lupe Fiasco
•             "Life Is Good" - Nas
•             "Undun" - The Roots
•             "God Forgives, I Don't" - Rick Ross
•             "Based on a T.R.U. Story" - 2 Chainz

Best Rap Song:
•             "Daughers" - Nas
•             "Lotus Flower Bomb" - Wale featuring Miguel
•             "Mercy" - Kanye West featuring Big Sean, Pusha T & 2 Chainz
•             "The Motto" - Drake featuring Lil Wayne
•             "N****s in Paris" - Jay-Z & Kanye West
•             "Young, Wild & Free" - Snoop Dogg & Wiz Khalifa featuring Bruno Mars

Best Country Album:
•             "Uncaged" - Zac Brown Band
•             "Hunter Hayes" - Hunter Hayes
•             "Living for a Song: A Tribute to Hank Cochran" - Jamey Johnson
•             "Four the Record" - Miranda Lambert
•             "The Time Jumpers" - The Time Jumpers

 Tembelea  Website ya Grammy kwa Nomination list nzima:

Monday, December 3, 2012

 Movie ya ‘Expendable 2’yaburuzwa tena mahakamani, ni baada ya mlipuko wa ukweli uliomuua actor mmoja na kumjeruhi vibaya actor mwingine
 Expendable two iliyowashirikisha action movie stars kibao wakiongozwa na Sylvester Stalonne (Rambo), Jean Claude Vanndamme, Jet-Li, Arnold ShwazNiger, na wengine, imekumbana na tatizo la kisheria.
Waandaaji na wawezeshaji wengine wanakabiliwa na mashtaka yanayotokana na scene ambayo haikwenda sawa na kupelekea mtu mmoja kupoteza maisha na mwingine kujeruhiwa vibaya.

Mtu mmoja anaejulikana kwa jina la Nuo Sun alijeruhiwa vibaya katika mlipuko ambao ulisababisha kifo cha muigizaji Kun Liu, ambapo kwa mara ya kwanza familia ya marehemu iliiburuza mahakamani ‘Expendable 2’ wakidai fidia mbalimbali ikiwa ni pamoja na fedha kiasi cha dola za marekani 25,000.

Taarifa za hivi karibuni zinasema Nuo Sun ambae alijeruhiwa vibaya na kupelekwa jijini Munich huko Ujerumani kwa matibabu akiwa chini ya the best specialist amewafungulia mashtaka waandaaji na washiriki wengine wa movie hiyo.

Katika mashitaka hayo yenye kurasa 12 Sun amedai kuwa, “mlipuko na similar extra-hazardous activities vilisababisha tukio la hatari juu ya rubber boat wakati wa kushoot sehemu ya pili ya filamu hiyo October 27, 2011.

“Kwa uzembe wa moja kwa moja wa washitakiwa, kutojali, na matendo kinyume na sheria, mlalamikaji aliumia na kupata majeraha katika afya yake, uwezo wa kufanya kazi, mshituko wa kiasi kikubwa na majeraha katika mfumo wake wa fahamu, shingo, kichwa, mwili, mikono na miguu, majeraha yote haya yanaweza kuwa ya kudumu, na majeraha haya yamesababisha na yanaendelea kusababisha madhara katika fahamu zake na mwili wake kwa ujumla. Hivyo mlalamikaji anadai fidia .” Haya ni baadhi ya maandishi yanayopatikana kwenye faili la mashtaka lenye kurasa 12.

Akiwakilishwa na Robert M. Klein, Sun anadai fidia ya hasara ya kipato chake kwa wakati uliopita, uliopo na ujao. Lakini pia anadai fidia ya jumla zaidi ya $25,000, gharama za matibabu ya wakati uliopita, uliopo na hata baadae, gharama za kuendesha kesi na mengine ambayo mahakama itaamua.

Baada ya mlipuko huo ulioua mmoja kati ya actors wa movie hiyo na kumjeruhi vibaya Sun, uongozi na watayarishaji wa movie hiyo walitoa tamko kuomba radhi na kuwaitakia pole familia ya marehemu na vilevile kuendelea kusapoti kwa karibu sana familia na kumhudumia Sun akiwa hospitalini.

Hata hivyo Sun alikanusha kauli iliyotolewa na waandaaji hao kuwa Jet-Li alikuwa pia karibu na mlipuko huo, na kusema hakuna star yoyote aliyekuwa karibu na mlipuko huo

Chanzo Leotainment

Sunday, December 2, 2012

GAGA APOSTI PICHA AKIWA NA SIMBA SOUTH AFRICA


Lady Gaga amepata shavu la kutalii vivutio vya Afrika baada ya kudondoka Afrika Kusini alikokuwa kwa ajili ya tour yake na kutembelea mbuga za wanyama

Lady Gaga alionesha furaha yake ya kukutana uso kwa uso na kupiga picha na wanyama wakali simba na kupost picha hizo kwenye ukurasa wake wa twitter akiwa amevalia nguo zenye rangi yanayoendana na mzingira ya hapo nyuma yake wakionekana simba kadhaa wakiwa wamejiachia kwenye nyasi kama






Gaga aliposti picha zake zikiwa na yanayosema SAFARI PICTURE: na yanayoeleza umbali wa futi 10 kutoka pale walipo simba13 na watoto 2.

‘The bad Romance singer’alipost picha kupitia twitter inayoonyesha akiwa kavaa mavazi ambayo yanaendana kabisa na nature ya pale alipo na  vile hakuna binadamu maeneo yale. "Nilispend nao takribani dakika 30 na kupiga picha!”

“hii niliichukuwa kama futi 5 hivi kutoka kwa simba jike, isn’t she beautiful!”

“simba walijiskia poa hata wakaamka at one point na wakatufanya kuwasogelea zaidi.”

Saturday, December 1, 2012

WANANDOA HATARINI KUAMBUKIZWA VVU

Watu Waanoishi Katika Ndoa Wapo Katika Hatari Kubwa ya Maambukizi ya Virusi vya Ukimwi Kwa Asilimia 70 Kwa Kuwa Ndio Wanaoongoza Kutoka Nje ya Ndoa Hivyo Kusababisha Ongozeko la WatotoYatima

Hayo yamesemwa na Mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa wa Njombe Kapteni Mstaafu Aseri Msangi  Katika Maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani Yaliyofanyika Katika kata ya Mji Mwema Katika Halmashauri ya Wilaya ya Njombe

Akizitaja Sababu  za Ongezeko la maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi Mkuu Huyo Amesema Kuwa Ngono Zembe Ulevi, Kurithi Wajane na Wagane na Wanaume Kutotahiriwa. Pia Amezitaja Sababu Zingine Kuwa Ni Matumizi mabaya ya Nyumba za Kulala Wageni Ufahamu Mdogo Juu ya Matumizi ya Kinga na Matumizi Hafifu ya Kinga.

Pia Mkuu wa Mkoa Amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kuwanyang'anya Leseni Wamiliki wa Nyumba za Kulala Wageni Watakaokiuka Maadili ya Leseni Hizo

Kulingana na Katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977 Watu Wanaoishi na Virusi vya Ukimwi na Ukimwi Wana Haki Sawa na Wale Ambao Hawajaambukizwa Hivyo Kumnyanyapaa Mwenye Virusi vya Ukimwi ni Kosa Kisheria.

Amesema Lengo la Maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Dunia ni Kupata Fursa ya Kutafakari Kwa Undani Ukubwa wa Tatizo la VVU na Ukimwi na Madhara ya Janga Hili kwa Jamii Zetu na Kujua mikakati, Mafanikio na Changamoto za Mapambano Dhidi ya Ukimwi.

Akisoma Risala Mbele ya Mgeni Rasmi Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Amesema Kuwa Takwimu Zinaonesha Kuwa Jumla ya Watu 2161 Kati ya Watu 21053 Sawa na Asilimia 10 ya Watu Walijitokeza kupima kwa Hiari katika Kipindi cha Kuanzia Julai 2011 hadi Juni 2012  Walikutwa na Maambukizi  
   

Friday, November 30, 2012

SERIKALI YATAKIWA KUONGEZA BAJETI YA MAHAKAMA

 Serikali Imetakiwa  Kuongeza  Bajeti Katika Idara ya Mahakama  Hapa Nchini Ili Kuepuka  Vitendo Vya Rushwa Kwa  Wananchi  Waendeshaji  Mahakama.

Akizungunza na Kituo  Hiki Mwanasheria John Owegi  Ambaye ni Wakili wa Kujitegemea Mkoani Njombe Anesema Ufinyu Wa Bajeti  Katika Mahakama Unapelekea Kuwepo Kwa Mianya ya Rushwa na Kukosesha Haki Kwa  Mtuhumiwa Hali Inayo Pelekea Kupindishwa Kwa Sheria Miongoni Mwa Jamii.

Bwana Owegi Amesema Kuwa Hali Hiyo Inapelekea Kuvunjika Kwa Amani Hapa Nchini  Kutokana na Baadhi ya  Mahakama  Kutotenda Haki Katika Maamuzi ya Kazi na Hivyo Kuleta  Mpasuko  wa Kisheria Kwa Wananchi.

Aidha Amewataka Wananchi Kuwatumia  Mawakili Wa Kujitegemea Katika  Kazi Zao Kutokana  na Mahakama  Kushindwa  Kutenda Haki  Katika Maamuzi  Hali Inayopelekea Kuhukumiwa Kwa Mtu Ambaye  Wakati Mwingine Hana Hatia.

Akijibu Swali Lililouliza Juu ya  Utaratibu Wa  Kutumia Wakilia wa Kujitegemea  Wakili Owegi Amewataka Wananchi Kuondoa  Hofu Juu ya Huduma Zao Kwani Wakati Mwingine Wao Hutoa Huduna ya Kisheria Bure  Kulingana  na Ukubwa wa Kasi  na Kwamba Wao Wapo Kwaajili ya Jamii Hivyo Kinachopelekea  Kumchaji mteja ni  kutokana na wao kulipia leseni.

SERIKALI INATARAJIA KUZINDUA CHANJO MPYA MBILI ZA WATOTO WACHANGA

Serikali inatarajia kuzindua chanjo mpya mbili za watoto wachanga ikiwemo chanjo ya kuzuia kuharisha na chanjo ya kichomi NIMONIA ugonjwa unaosababishwa na bacteria anayeitwa STREPTOCOCCUS PNEUMONIAE Ulioonekana kuwakumba watoto wadogo.

Akifungua kikao cha semina ya afya ya Mkoa wa Njombe iliyolenga kutoa elimu juu ya chanjo hizo mkuu wa mkoa
 wa Njombe Captain Mstaafu Asseri Msangi amewataka wazazi kumpeleka mtoto kupata chanjo hizo kabla ya siku saba baada ya kuzaliwa kutokana na athari zinazoweza kujitokeza kwa mtoto kutokana na kukosa chanjo hizo.

Captain Msangi ameeleza kuwa wataalamu wa afya hawana budi kutoa elimu ya kiwango cha juu kwa wauuguzi watakao husika na zoezi hilo mara baada ya kuzinduliwa rasmi kwani chanjo hususani za sindano zinahitaji umakini mkubwa wakati wa kumchoma mtoto.


Akitoa elimu hiyo kwa  wadau mbalimbali wa afya katika ngazi ya mkoa wa Njombe Kaimu Mganga mkuu wa Mkoa wa Njombe Dokta Thomas Lujuo amesema kuwa takwimu zinaonesha kuwa Ugonjwa wa Kuhara Umekuwa Ukishika Nafasi ya Pili Kati ya Magonjwa Yanayoongoza Kwa Kusababisha Vifo Vya Watoto Kwa Asilimia 17 Huku Ugonjwa wa Nimonia Ukisababisha Vifo Kwa Asilimia 14 Ulimwenguni Kote.

Dokta Lujuo ameeleza baadhi ya dalili za ugonjwa wa NIMONIA Kuwa ni pamoja na mtoto kupumua kwa shida,kukohoa,homa na kushindwa kula au kunyonya.

Aidha Dokta huyo amesema NIMONIA husababisha vifo zaidi ya milioni 1.4 duniani kwa watoto waliochini ya umri wa miaka mitano huku kwa nchi za afrika,NIMONIA huchangia asilimia 18% ya watoto waliochini ya umri wa miaka  mitano.

Amesema Kuwa Chanjo Hiyo Ni Kampeni ya Kitaifa Inayotokana na Tafiti za Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Kuonesha kuwa Watoto wengi wanapata Magonjwa ya Kuhara Na Nimonia .



Thursday, November 29, 2012

Wednesday, November 28, 2012

WAFANYABIASHARA WALALAMIKIA KODI YA MISITU

Msako wa kodi zitokanazo na misitu uliofanyika kuanzia novemba 26 mwaka huu mjini Njombe umepelekea malalamiko makubwa kwa wafanyabiashara kuilalamikia serikali kwa kuendesha zoezi hilo kwa kutumia nguvu.

 Hali hiyo imepelekea wafanyabiashara wa bidhaa zitokanazo na misitu ya maliasili kuingiwa na hofu kubwa kutokana na msako huo uliofanyika kwa kutumia jeshi la polisi ambao wamekuwa wakitumia silaha za moto huku wakisema zoezi hilo limefanika ghafla bila mawasiliano.

 Wakizungumza kwenye mkutano uliofanyika leo katika ukumbi wa Turbo baina ya Wafanyabiashara hao na maliasili wamesema kuwa hatua ya kuwakamata kulipia kodi bila kuangalia uwezo wa biashara ni kuwanyanyasa na kuwanyima haki za kufahamu sheria ya tozo la kodi hizo.

Wamesema kuwa kitendo cha Halmashauri ya mji wa NJOMBE Kuanza kuwakamata na kuwatoza kiasi cha zaidi ya shilingi laki tatu bila kuangalia ni biashara gani inafanyika ni kuto watndea haki hali iliyopelekea kuwasilisha malalamiko yao kwa diwani wao.

Kufuatia hali hiyo afisa misitu wa halmashauri ya mji wa Njombe Bwana GEOFREY MWAMAKUNGE amelazimika kutoa elimu na kuwaelimisha juu ya kodi hizo ambazo wanatakiwa kuzilipa kila Julai mosi huku akisema kodi hizo zinatozwa kulingana na uwezo wa biashara.

Bwana Mwamakunge ameeleza kuwa kilichopelekea kuanza kwa msako huo ni kutokana na kufika kwa wakaguzi toka makao makuu ambao wameanza operation ya nchi nzima kuwakamata na kuwatoza wale wote ambao hawajalipia kodi za biashara zao kama Mafundi selemala,wauza mkaa,Mbao na waganga wa tiba asili.

Kwa upande wake diwani wa kata ya Njombe Mjini bwana Lupyana Fute ambaye amelazimika kuwaita wataalamu hao mara baada ya kufikishiwa malalamiko toka kwa wananchi wake amesema kuwa serikali inatakiwa kuweka elimu mbele kabla ya kuanzisha msako ili kuwapa mwanga wa kutambua umuhimu wa kulipa kodi hizo.

 Aidha bwana Fute amewataka wafanyabiashara hao wanaotumia bidhaa zitokanazo na miti mjini Njombe kuanzisha umoja wao ili kupunguza gharama ya makusanyo kodi pindi msako unapoanza na kumkumba mtu mmoja mmoja.

Tuesday, November 27, 2012

VIONGOZI WILAYA YA LUDEWA WATAKIWA KUSIMAMIA MAPATO

Viongozi na Watendaji Katika Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa Hususani Mkurugenzi na Mkuu wa Wilaya Wakiwemo Wakuu wa Idara Mbalimbali Wametakiwa Kusimamia Mapato Kikamilifu ILi Kuiongozea Halmashauri ya Wilaya Hiyo Mapato ya Kutosha

Maagizo Hayo Yametolewa na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Kapteni Mstaafu Aseri Msangi Baada ya Kupokea Taarifa ya Wilaya ya Ludewa Alipowasili Wilayani Hapa Kwa Ziara ya Siku Tatu Ambayo Imelenga Maeneo ya Kata Zote za Tarafa ya Mwambao

 Mkuu Huyo Wa Mkoa Alifikia Hatua Hiyo Baada ya Kubaini Wilaya Hiyo Kudumaa na Kukosa Mabadiliko Katika Nyanja Mbalimbali Ikiwemo Kilimo, Uvuvi na Biashara

Kwa Mujibu wa Ratiba, Leo Mkuu wa Mkoa Ataweka Jiwe la Msingi Katika Ofisi ya Kata ya Makonde na Kufanya Mikutano ya Hadhara Katika Kijiji cha Makonde na Lisuma. Kesho Novemba 28 Mkuu wa Mkoa Ataweka Jiwe la Msingi Katika Ujenzi wa Nyumba ya Mganga Kata ya Kilondo na Kufanya Mkuktano wa Hadhara na Kisha Kuweka Jiwe la Msingi Ofisi ya Kata ya Lundila na Kufuatiwa na Mkutano wa Hadhara

 Hata Hivyo Mkuu Huyo wa Mkoa Amewaagiza Wakuu wa Idara Hao Kusimamia na Kufuatilia na Kuacha Kukaa Maofini Badala Yake Waende Vijijini Kuwahimiza Wananchi Katika Shughuli za Maendeleo Mkuu wa Mkoa Anategemea Kumaliza Ziara Yake Novemba 29 Mwaka Huu Ambapo Atapitia Mkoani Mbeya, Kyela, Matema na Kisha Kurudi Mkoani Njombe.

Tuesday, November 13, 2012

MATOKEO YA WAJUMBE WA NEC YAVUJA DODOMA

MATOKEO ya uchaguzi wa wajumbe wa NEC Uliofanyika juzi mjini Dodoma katika mkutano wa nane wa (CCM) yamevuja.

 Mwenyekiti wa chama hicho , Rais Jakaya Kikwete alitangaza jana kuwa matokeo hayo yatatangazwa leo pamoja na matokeo ya nafasi za Makamu Mwenyekiti lakini cha ajabu jana mchana zaidi ya asiliamia 90 ya wajumbe walisha jua matokeo hayo na kwa upande wa wagombea wa bara yakiwekwa na idadi ya kura zao huku Steven Wasira Akiongoza kwa kura nyingi.

 Kwa Upande wa Zanzibar Wanaodaiwa Kushinda Uchaguzi Huo ni Mbunge wa Uzini, Mohamed Seif Khatib; Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hussein Ali Mwinyi, Waziri wa Fedha Zanzibar, Omar Yussuf Mzee, Abdulhakim Chasama na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Shamsi Vuai Nahodha.

Wengine ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan, Khadija Hassan Aboud, Bhaguanji Mansuria, Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa na Khamis Mbeto.

 Wanaodaiwa kushinda Bara Majina na kura walizopata katika mabano ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wassira aliyeongoza kundi hilo kwa kupata kura 2,135, Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba (2,093), Mwekahazina wa CCM, Mwigulu Nchemba (1,967), na Katibu wa UVCCM, Martine Shigela (1,824)

 Wengine ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi (1,805), Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa, Bernard Membe (1,455), Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Mathayo David Mathayo (1,414), Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Jackson Msome (1,207), Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama (1,174) pamoja na Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana  na Michezo, Fenela Mukangara (984).

Sunday, October 28, 2012

Wateja wa mafuta wakisubiri foleni ya mafuta Mkoani Njombe, Nishati Hiyo Imekuwa kitendendawili kwa siku za hivi karibuni.

Saturday, October 13, 2012

MRADI WA KILIMO WAZINDULIWA WILAYANI WANGING'OMBE



Mradi wa mwelekeo wa maendeleo ya kilimo katika shirika la maendeleo ya kilimo mkoa wa Njombe la NADO  unaoitwa NADO IN FOCUS leo umezinduliwa rasmi Wilayani Wanging'ombe.

Akizindua mradi huo kwa niaba ya mkuu wa Mkoa wa Njombe Afisa Biashara wa mkoa wa Njombe bwana George Lupembe amepongeza jitihada kubwa zinazofanywa na shirika la NADO Katika kuwakomboa wakulima kwa kujiinusuru na kipato kupitia kilimo ikiwa ni njia mojawapo ya kutekeleza Sera ya KILIMO KWANZA hapa Nchini.

Bwana Lupembe amesema kuwa pamoja na kuzindua mradi huo ulioambatana na uzinduzi wa vyombo vya usafiri kwa maafisa kilimo lakini serikali haina budi kuendeleza ushirikiano na shirika hilo ili kupunguza ukali wa maisha kwa wakulima mkoani Njombe

Friday, October 12, 2012

WAFANYABIASHARA WALAZIMIKA KUAHIRISHA KIKAO NA MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA

Baadhi ya Wafanyabiashara Mjini Njombe Wakiwa Nje ya Ofisi ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe



 Wafanyabiashara Mijini Njombe Wamelazimika Kuahirisha Kikao Kilichopangwa Kufanyika Saa 3 Asubuhi Hii Leo na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Bwa. Valency Kabelege Baada ya Mwenyekiti Huyo Kutoa Taarifa ya Kuwa na Dharura Ndani ya Muda wa Kikao Hicho.

 Kikao Kilichopangwa Kufanyika Saa 3 Asubuhi Hii Leo na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Bwa. Valency Kabelege Baada ya Mwenyekiti Huyo Kutoa Taarifa ya Kuwa na Dharura Ndani ya Muda wa Kikao Hicho.

Akitoa Taarifa Hiyo Kwa Njia ya Simu, Bwa. Kabelege Alisema Kuwa Yupo Kwenye Kikao Lakini Muda Mfupi Baadae Alitoa Taarifa Tofauti Kupita Kwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe Kuwa Mtoto Wake ni Mgonjwa Hivyo Hatoweza Kuhudhuria.

Kikao Hicho Kimeahirishwa Mpaka Tarehe 16 Mwezi Huu Saa 3 Asubuhi Kikao Ambacho Kitawahusisha Wawakilishi wa Wafanyabiashara Hao Wakiongozwa na Mwenyekiti Patrick Msigwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Bwa. Kabelege.

Siku ya Jumanne ya Tarehe 09 Mwezi Huu Wafanyabiashara Hao Walifanya Kikao na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe Bwana Edwin Mwanzinga Wakiwasilisha Madai Yao Kwa Serikali Kwa Kushindwa Kulipwa Madai Yao Kwa Wakati.

Katika Kikao Hicho Kilichopita Bwana Mwanzinga Alikiri Kuwepo Kwa Tatizo Hilo na Kuahidi Kulitolea Ufafanuzi Siku Ya Tarehe 13 Jumamosi Mwezi Huu Saa 6 Mchana Katika Ukumbi wa PASTO Mjini Njombe.

Thursday, October 11, 2012

HALI YA UPATIKANAJI WA MAFUTA YAREJEA KAWAIDA MJINI NJOMBE



Hali ya Upatikanaji wa Mafuta Katika Mji wa Njombe Imerejea Katika Hali ya Kawaida Baada ya Siku Kadhaa Zilizopita Kutopatikana kwa Nishati Hiyo Muhimu Hasa Mafuta Aina ya Dizeli.

Akiongea na Mwandishi wa Blog Hii, Meneja wa Kituo cha Kuuza Mafuta cha Ndime, Clement Mwauling'ombe Mtewele amesema kuwa Mafuta aina ya Dizeli yameanza Kupatikana  Tangu Jana na kiasi cha mafuta kilichopo kwa sasa kinaridhisha
                                                                                       
                                                                                      

kutegemeana na mahitaji ya wateja wake.

Pia Bwana Mtewele Hakusita Kuimwagia Sifa
Uplands Radio Kwa Kutoa Matangazo Na Vipindi
Vizuri Vya Kuburudisha na Kuelimisha Umma

Kwa upande wake Msemaji wa Kituo cha Gapco, Bi Joyce Fute Amesema mafuta Yanapatikana kwa Wingi Kituoni Hapo Tangu Jana. Pia Bi Fute             Amewaondoa Hofu Watumiaji Wa Nishati Hiyo Kwa Kuwa Wana Hifadhi ya Kutosha kwa Sasa. Pamoja na Kuwa Vituo Vingi Kuonekana
 Kupatikana             
Mafuta Hivi Sasa Lakini Baadhi ya Vituo         Vimeonekana  Kufungwa
Muda Wote Kama Vile                                             
 Oilcom na Wahudumu Wake Kutopatikana                  

Tuesday, October 2, 2012

Wanafunzi 25 wauawa na Boko Haram

 2 Oktoba, 2012 -

Abubakar Shekahu kiongozi wa kundi la Boko Haram

Zaidi ya wanafunzi 25 wameuawa kwa kupigwa risasi katika eneo la Mubi, Kaskazini Mashariki mwa Nigeria.
Polisi wamefahamisha  kuwa shambulizi hilo limetokea katika mabweni yao mbali kidogo na chuo cha ufundi anuwai cha Mubi.
Mhadhiri mmoja amefahamisha kuwa wanafunzi 40 wameuawa lakini bado taarifa hizo hazijathibitishwa.
Mauaji haya yanakuja siku chache baada ya operesheni kali kufanywa dhidi ya kundi la wapiganaji wa kiisilamu la Boko Haram mjini humo.
Aidha mhadhiri ambaye hakutaka kutajwa, aliambia  kwamba wanafunzi waliamrishwa kupanga foleni na kusema majina yao mmoja baada ya mwingine kabla ya kuuawa.
Haijulikani kwa nini baadhi waliuawa na wengine kuachwa, baadhi ya wale waliouawa ni waisilamu.
"kila mtu anaogopa na wamejifungia vyumbani," alisema mhadhiri huyo.
Aliongeza kuwa wanafunzi sasa wameanza kuuhama mji huo. Inasemekana wameweka majani ya rangi ya kijani kibichi kwenye magari yao kama ishara kuwa hawaungi mkono upande wowote.
Wapiganaji wa Boko Haram wanaopigana wakitaka sheria za kiisilamu kutumika, wamewaua zaidi ya watu 1,000 Kaskazini mwa Nigeria.

Tuesday, September 25, 2012

Daktari: Serikali inahusika ARV bandia  

ATAKA IJIHOJI  IJE NA MAJIBU, AELEZA ATHARI ZAKE, NAIBU WAZIRI ATAKA IPEWE MUDA ZAIDI KUCHUNGUZA TATI
WAKATI utata ukiendelea kugubika usambazwaji wa dawa bandia za kupunguza makali ya virusi vya Ukimwi (ARV), daktari katika Kitengo cha Ukimwi, Dar es Salaam ameitaka Serikali kujichunguza yenyewe, kwa kuwa dawa hizo hazisambazwi na watu binafsi.

Daktari huyo, Charles Lyimo ambaye ni Mkuu wa Idara ya Dawa katika Kitengo cha Ukimwi Hospitali ya Amana, alisema jana kuwa hakuna sababu ya kutafuta mchawi kwenye tatizo hilo; Serikali inahusika.

“Siyo rahisi kujua kwamba hii ni dawa halisi au bandia, lakini tuna uhakika na dawa tunazotumia kwa sababu zinaagizwa na Serikali peke yake. Hakuna mtu binafsi aliyepewa tenda (zabuni) ya kuziagiza,” alisema Dk Lyimo.
Dk Lyimo alisema awali, dawa hizo zilikuwa zikiagizwa kutoka Marekani, lakini baadaye utaratibu huo ukabadilishwa na zikaanza kuagizwa kutoka India.

“…(Serikali) inapeleka oda kiwandani na ndiyo inayozigawa dawa hizo na kuzisambaza kupitia Bohari Kuu ya Dawa (MSD). Lakini pia dawa hizi zinatengenezwa Arusha kwenye kiwanda kilichopewa kibali na Serikali,” alisema Lyimo na kuongeza:

“Kama kuna dawa bandia, basi Serikali ijihoji. Kwanza mimi ninaposikia habari hizo huwa nacheka tu kwa sababu tangu sakata hili limeanza, wizara inajigongagonga tu… hawatuhusishi wala kutuuliza… na sisi tunaendelea tu kugawa dawa…”