Friday, August 25, 2017

Mkurugenzi Mkuu wa Samsung Lee Jae-yong ahukumiwa jela miaka mitano

Mahakama moja nchini Korea Kusini imemhukumu kifungo cha miaka mitano jela Mkurugenzi Mkuu na mrithi wa Samsung, Lee Jae-yong baada ya kutiwa hatiani kwa
rushwa na matumizi mabaya ya mali za umma.

Lee alishtakiwa kwa tuhuma za rushwa akidaiwa kutoa msaada wenye thamani ya Dola 36 milioni za Marekani kwa taasisi isiyo ya kiserikali inayoendeshwa na Choi Soon-sil ambaye ni rafiki wa Rais wa zamani wa Korea Kusini, Park Geun-hye kwa malengo ya kujipatia faida kisiasa.

Kutokana na tuhuma hizo za rushwa, Lee alikamatwa na kuwekwa kizuizini tangu Februari. Kashfa hiyo ilisababisha maandamano ya wananchi kumpinga Rais Park aliyeondolewa madarakani.

Mwanasheria wa Lee, Song Wu-cheol amesema kuwa wanatarajia kukata rufaa kupinga hukumu hiyo wakiamini mahakama inaweza kuitengua.

0 Comments:

Post a Comment