Samatta alipambana kwa dakika zote 65 kabla ya kubadilishwa, nafasi yake ikichukuliwa na mshambuliaji Mgiriki, Nikolaos Karelis ambaye naye hakuweza kwenda kubadili matokeo.
Hiyo inakuwa mechi ya 83 kwa Nahodha huyo wa Taifa Stars, Samatta tangu alipojiunga na Genk Januari mwaka 2016 akitokea TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
Na katika mechi hizo, Samatta, mshambuliaji wa zamani wa Mbagala Market, African Lyon na Simba za Tanzania, amefunga mabao 22 kwenye mashindano yote.
Kikosi cha AA Gent kilikuwa; Kalinic, Gigot, Verstraete, Christiansen/Chakvetadze dk79, Janga/Kalu dk45, Yaremchuk, Dejaegere/Andrijasevic dk45, Asare, Bronn, Simon na Foket.
KRC Genk; Vukovic, Uronen/Nastic dk43, Colley, Aidoo, Maehle, Seck, Malinovskyi, Pozuelo, Trossard, Samatta/Karelis dk65 na Ndongala/Buffel dk84.
0 Comments:
Post a Comment