Wednesday, April 18, 2018

Serikali Kuajiri Walimu 6,000 June

    Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), imesema hadi kufikia Juni 30 mwaka huu inatarajia kuajiri walimu 6,000 wa masomo ya Hisabati na Sayansi kwa ajili ya shule za sekondari nchini. Kauli hiyo ilitolewa jana bungeni na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais (Tamisemi),...

Mvua zaendelea kuleta madhara nchini

 Mvua zinazoendelea kunyesha sehemu mbali mbali nchini zimeendelea kuleta madhara mkoani Rukwa, ambapo zimesababisha uharibifu wa mashamba ya vyakula na kuharibu mazao. Hayo yamesemwa na Kamanda wa Polisi Mkoani Rukwa, George Kyando ambapo amesema kuwa mvua hizo zimezoa mazao kwenye...

Wachunguzi wa sumu Hatimaye Wameruhusiwa Kuingia Syria

Wachunguzi wa kimataifa leo Aprili 18 wameingia katika mji wa Syria uliokumbwa na kile kinachodaiwa kuwa ni shambulizi la sumu. Hata hivyo, wachunguzi hao wanaingia nchini humo ikiwa ni  siku kadhaa za kucheleweshwa na onyo kutoka kwa mataifa ya magharibi kuwa ushahidi muhimu huenda umeshaondolewa. Shirika ...

SAMATTA ABADILISHWA BAADA YA SAA MOJA GENK IKITOA SARE YA 0-0 UGENINI

MSHAMBULIAJI wa kimataifa Tanzania, Mbwana Ally Samatta usiku wa Jumanne amecheza kwa dakika ya 65, klabu yake, KRC Genk ikilazimisha sare ya 0-0 na wenyeji, AA Gent katika mchezo wa Ligi Daraja la Kwanza A Ubelgiji Uwanja wa Ghelamco-Arena mjini Gent. Samatta alipambana kwa dakika zote 65 kabla...

KILA LA HERI YANGA SC; MUNGU IBARIKI TIMU YETU IFUZU HATUA YA MAKUNDI KOMBE LA SHIRIKISHO

  YANGA SC inateremka Uwanja wa Hawassa mjini Hawassa, Ethiopia kuanzia Saa 10:00 jioni ya leo kwa saa za Tanzania kumenyana na Welaita Dicha ya Ethiopia katika mchezo wa marudiano wa mchujo kuwania tiketi ya hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika. Yanga inaingia kwenye mchezo wa leo,...

Monday, April 16, 2018

MSUVA AFUNGA MAWILI NA KUINUSURU JADIDA KUCHAPWA UGENINI LIGI YA MOROCCO

  WINGA wa kimataifa wa Tanzania, Simon Msuva leo amefunga mabao mawili timu yake, Difaa Hassan El Jadida ikilazimisha sare ya 3-3 ugenini katika mchezo wa Ligi Kuu ya Morocco dhidi ya wenyeji, Olympique de Khouribga Uwanja wa Phosphate mjini Khouribga. Matokeo hayo yanaiongezea pointi moja...

ZANZIBAR WAFUNGIWA KUSHIRIKI CECAFA U-17 KWA KUPELEKA WAKUBWA, SERENGETI YATOA SARE NA BURUNDI

  TIMU ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Zanzibar, Karume Boys imefungiwa mwaka mmoja kushiriki michuano ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge Cup U17 na kupigwa faini ya dola za Kimarekani 15,000 kwa kosa la kupeleka wachezaji waliozidi umri. Michuano ya CECAFA Challenge...

Sunday, April 15, 2018

Milio ya risasi inasikika katika vijiji vya Beni DRC

Tunapokea taarifa kwamba milio ya risasi na mizinga inasikika katika mji wa Beni kaskazini mashariki mwa Jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo. Duru za kuaminika zimesema waasi kutoka Uganda wa ADF wamezishambulia kambi kadhaa za jeshi la taifa hilo. Mapigano hayo yanaripotiwa katika vijiji vya Ngadi,...

Mvua kubwa Dar es Salaam yatatiza usafiri wa mabasi ya mwendokasi

Usafiri wa mabasi hayo umesitishwa kutokana na mafuriko eneo la Jangwani. Muandishi wa BBC Mjini Dar es Salaam anaeleza kuwa kila mvua kubwa inaponyesha huduma za mabasi hayo husitishwa kutokana na sababu kadhaa. Mojawapo ya sababu ni kufurika maji kwa njia ambazo mabasi hayo yanapitia na pia...

Sunday, April 8, 2018

Serikali Kuanzisha Kampeni Ya Jiongeze Tuwavushe Salama ili kupunguza vifo vya Mama na Mtoto

Rais Mstaafu Jakaya Kikwete amesema matatizo ambayo yanatokana na uzazi yapo ambayo yanaweza kuzuilika na kuhimiza wadau kushirikiana na Serikali kwa lengo la kuendelea kupunguza vifo vya mama mjazito na mtoto. Pia ametoa pongezi kwa hatua zinazochukuliwa na Taasisi ya Childbirth Survival International(CSI)...

Thursday, April 5, 2018

Wednesday, April 4, 2018

TWIGA STARS WABANWA NYUMBANI NA ZAMBIA, SARE 3-3 KUFUZU FAINALI ZA AFRIKA GHANA 2018

     TIMU ya soka ya Taifa ya Wanawake (Twiga Stars) imejiweka vibaya katika kampeni ya kusaka tiketi ya kushiriki fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AWC) Ghana Novemba mwaka huu kwa kutoka sare ya mabao 3-3 dhidi ya wenzao wa Zambia (Shepolopolo) katika mechi iliyofanyika...

Hotuba ya Kambi ya upinzani kuhusu bajeti ya ofisi ya Waziri Mkuu, haitasomwa bungeni

Hotuba ya Kambi ya upinzani kuhusu bajeti ya ofisi ya Waziri Mkuu, haitasomwa bungeni baada ya kambi hiyo kuchelewa kuiwasilisha. Hayo yameelezwa leo, Aprili 4 na Naibu Spika Dk Tulia Ackson dakika chache kabla ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, kusoma bajeti yake. “Kwa maelekezo yaliyotolewa na...