Tuesday, September 25, 2012

Daktari: Serikali inahusika ARV bandia  

ATAKA IJIHOJI  IJE NA MAJIBU, AELEZA ATHARI ZAKE, NAIBU WAZIRI ATAKA IPEWE MUDA ZAIDI KUCHUNGUZA TATI
WAKATI utata ukiendelea kugubika usambazwaji wa dawa bandia za kupunguza makali ya virusi vya Ukimwi (ARV), daktari katika Kitengo cha Ukimwi, Dar es Salaam ameitaka Serikali kujichunguza yenyewe, kwa kuwa dawa hizo hazisambazwi na watu binafsi.

Daktari huyo, Charles Lyimo ambaye ni Mkuu wa Idara ya Dawa katika Kitengo cha Ukimwi Hospitali ya Amana, alisema jana kuwa hakuna sababu ya kutafuta mchawi kwenye tatizo hilo; Serikali inahusika.

“Siyo rahisi kujua kwamba hii ni dawa halisi au bandia, lakini tuna uhakika na dawa tunazotumia kwa sababu zinaagizwa na Serikali peke yake. Hakuna mtu binafsi aliyepewa tenda (zabuni) ya kuziagiza,” alisema Dk Lyimo.
Dk Lyimo alisema awali, dawa hizo zilikuwa zikiagizwa kutoka Marekani, lakini baadaye utaratibu huo ukabadilishwa na zikaanza kuagizwa kutoka India.

“…(Serikali) inapeleka oda kiwandani na ndiyo inayozigawa dawa hizo na kuzisambaza kupitia Bohari Kuu ya Dawa (MSD). Lakini pia dawa hizi zinatengenezwa Arusha kwenye kiwanda kilichopewa kibali na Serikali,” alisema Lyimo na kuongeza:

“Kama kuna dawa bandia, basi Serikali ijihoji. Kwanza mimi ninaposikia habari hizo huwa nacheka tu kwa sababu tangu sakata hili limeanza, wizara inajigongagonga tu… hawatuhusishi wala kutuuliza… na sisi tunaendelea tu kugawa dawa…”

Sunday, September 16, 2012

                                   Pipi sasa ni mama 

Pipi baada ya kujifungua
Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Pipi ambaye alifanya vizuri katika wimbo wa "Njia Panda" alioshirikiana na Barnaba amebahatika kuitwa Mama baada ya kujifunga mtoto wa kiume aliyempa jina Kingston siku ya tarehe 14 septemba mwaka huu.


    Baada ya kujifungua Pipi alimshukur Mungu kwa kutimiza lake la kuzaa kwa uchungu, lakini pia hakusita kumshukuru mama yake


     Tunakutakia malezi mema na yenye maadili kwa mtoto wako Kingston kwani MKONO ULEAO MWANA NDIO UJENGAO TAIFA.

Wednesday, September 12, 2012

Home » » Muuaji Wa Mwangosi Afikishwa Mahakamani Iringa

Muuaji Wa Mwangosi Afikishwa Mahakamani Iringa



Baadhi ya wanahabari wakitoka mahakamani


Askari anayetuhumiwa kumuua Daudi Mwangosi leo amefikishwa katika Mahakama ya wilaya ya mkoa wa Iringa na kusomewa mashitakata yake. Huku akiwa chini ya ulinzi mkali ambao ulifanya wanahabari waliofika mahakamani kujitahid kupata picha kwa ugumu.
Akisoma mashtaka mbele ya hakimu mkazi mwandamizi wa mahakama ya wilaya Daines lymo mwendesha mashtaka ameeleza kuwa mtuhumiwa anaitwa Pacificus Cleophase Simon (23)

Witness aja na solution kwa matatizo ya nguvu za k...

 Witness aja na solution kwa matatizo ya nguvu za k...: Marafiki wa rapper wa kike nchini, Witness kupitia Facebook husasani wale wa kiume, wamepata somo la bure la jinsi la kuongeza nguvu za kiume
Marafiki wa rapper wa kike nchini, Witness kupitia Facebook husasani wale wa kiume, wamepata somo la bure la jinsi la kuongeza nguvu za kiume.

Hivi ndivyo alivyoandika:

Tsup my pipo, leo ninapenda kutumia facebook vizuri kwa kuzungumzia kazi ya madini ya zinc mwilini na yana patikana katika vyakula vya aina gani na yanaweza kuwa destroyed madini ya zinc yanapatikana haswa kwnye,cereals,nyama aina ya offal,kaa,pweza,ngisi,maharagwe,yeast,uyoga,mbegu za maboga alizeti pamoja na karanga korosho haswa brazilian nuts ina saidia sna kutibu vidonda naturally ndo maana watu wnye madini ya kutosha ya zinc mwililni huwa wanapona haraka kuliko wengine kwa kuwa miiili yetu iliumbwa kujiponya yenyewe, endapo ukaipa lishe bora vitamins na minerals za kutosha, pia husaidia kwenye mental alertness,ngozi kufunctioni zuri hata vichunusi meno na pia husaidia watu wenye matatizo ya manii kama ni ndogo na kushindwa kuzalisha mbegu za kutosha, huongeza uwezo na hamu ya kuchuja nafaka kwa wanaume na wanawake na kuongeza ufanisi wa afya ya viungo vya uzazi na endapo madini haya yakiongezwa na vitamins za nyingine yanaweza kutumika kwa kuondolea sumu mwilini na kusaidia mfumo wa chakula kufunction vizuri.

Kwa hiyo fikiria kaka kila unapo chuja nafaka ni unamwaga 5mg zinc na ukichuja bao tatu yamaanisha umepoteza zinc kiasi gani? hebu tujiulize kila siku unakamua ngapi? na je unakula hivi vitu kweli? ama ndo unaviskia bombani? mwenzenu cassanova alikuwa akila pweza angalau vikamba vyake hamsini kila asubuhi ili kumpatia nguvu na uwezo zaidi wa kuchuja nafaka wewe je? Kama huwezi kwa mtindo huo nipigie nikupe solution 0753 320 009 much love!...

Tuesday, September 11, 2012

TEC wachangia maoni kuelekea siku ya maadhimisho Tabaka Anga Hewa

           Wanafunzi wa chuo cha Tanzania e College jana walifanya intavyuu kuchangia maoni yao kuhusiana na mkutano wa 14 wa kimataifa wa Tabaka Anga Hewa unaoendelea Arusha. Tanzania imepata heshima ya kuandaa mkutano ikiwa ni sehemu ya kujadili matatizo na madhara yatokanayo na uharibifu wa anga hewa.
            Katika intavyuu hiyo iliyofanya na mwandishi wa habari wa TBC TAIFA, Musa Twangilo, wanafunzi hao walieleza sababu zinazopelekea kuharibu tabaka la Anga Hewa ambapo kunachangia madhara makubwa kwa viumbe hai hapa duniani.
             Wanafunzi hao walizitaja sababu hizo kuwa ni pamoja na ongezeko la viwanda vinavyozalisha moshi wenye kemikali zinazopelekea mvua za asidi (Acidic Rains) na ukataji wa miti hovyo. Pia wataja madhara yake kuwa ni kuongezeka kwa joto, mabadiliko ya majira ya mvua na ukame. Walioingeza madhara mengine kuwa ni magonjwa yatokanayo ongezeko la joto, kupotea kwa baadhi ya viumbe hai na mvua zisizo tarajiwa.
             Siku ya Tabaka Anga Hewa huadhimishwa kila mwaka tarehe 16 mwezi Septemba duniani kote kwa ajili ya kuhamasisha utunzaji wa mazingira ili kutunza tabaka anga hewa.