Saturday, October 13, 2012

MRADI WA KILIMO WAZINDULIWA WILAYANI WANGING'OMBE



Mradi wa mwelekeo wa maendeleo ya kilimo katika shirika la maendeleo ya kilimo mkoa wa Njombe la NADO  unaoitwa NADO IN FOCUS leo umezinduliwa rasmi Wilayani Wanging'ombe.

Akizindua mradi huo kwa niaba ya mkuu wa Mkoa wa Njombe Afisa Biashara wa mkoa wa Njombe bwana George Lupembe amepongeza jitihada kubwa zinazofanywa na shirika la NADO Katika kuwakomboa wakulima kwa kujiinusuru na kipato kupitia kilimo ikiwa ni njia mojawapo ya kutekeleza Sera ya KILIMO KWANZA hapa Nchini.

Bwana Lupembe amesema kuwa pamoja na kuzindua mradi huo ulioambatana na uzinduzi wa vyombo vya usafiri kwa maafisa kilimo lakini serikali haina budi kuendeleza ushirikiano na shirika hilo ili kupunguza ukali wa maisha kwa wakulima mkoani Njombe
.

Afisa huyo wa biashara katika mkoa wa Njombe aliyemwakilisha mkuu wa mkoa wa Njombe Captain Mstaafu Asseri Msangi amewataka wakulima katika shirika la NADO kumuunga mkono mkulima ambaye ni mzalishaji na msambazaji wa mbegu  za mazao katika wilaya ya Wanging'ombe bwana Njogela mkulima wa kijiji cha Chalowe kwa kuzinunua ili kuendana na kasi ya kilimo katika Halmashauri zote za mkoa wa Njombe.

Akitoa taarifa ya shirika hilo  la NADO pamoja na mradi huo Mkurugenzi wa shirika hilo bwana John Wihallah amesema kuwa Shirika hilo ni matokeo ya mwendelezo wa umoja wa vikundi vya maendeleo katika vijiji vya Sakalenga,Palangawanu,Chalowe na Itulahumbavilivyoanza kufanya shughuli za  maendeleo ya jamii na MS Tanzania mwaka 1996 kwa ubia.

Wihallaha amesema mradi huo uliozinduliwa rasmi leo umefadhiliwa na shirika la maendeleo ya kilimo la Denmark na Asia utakao kuwa na kipindi cha miaka mitatu wenye gharama zisizo pungua  shilingi bilioni tatu kwa ajili ya mafunzo ya mazao ya mazao ya Alizeti,Maharage,Mahindi,Kabeji,Nyanya na viazi mviringo ukiwa na lengo la kuwafikia wakulima 9000 katika vijiji 200 ifikapo 2015.

Mradi huo umeambatana na uanzishwaji SACCOS,Darasa la kompyuta,utengenezaji wa Batiki na sabuni,usindikaji wa matunda,Mbogamboga na vyombo vya usafiri kama pikipiki zenye gharama ya shilingi milioni 35 pamoja na usajili kuwa za NADO likiwemo gari la mradi na vitendea kazi vya ofisi na mawasiliano.

0 Comments:

Post a Comment