Monday, September 25, 2017

MSIGWA AACHIIWA

Mbunge wa Iringa Mjini (CHADEMA), Mch. Peter Msigwa ameachiwa huru kwa dhamana jana usiku baada ya kukamatwa akiwa kwenye mkutano wa hadhara.
Msigwa ameachiwa baada ya kudhaminiwa na wadhamini wawili ambao ni Alex Kimbe pamoja na Mwenyekiti wa Bavicha Iringa Leonce Marto , saa nne usiku 

Msigwa alishushwa jukwaani jana jioni na jeshi la polisi akiwa anahutubia mkutano wa hadhara katika kata ya Mlandege Manispaa ya Iringa ambapo alikamatwa kwa kutuhumiwa kufanya uchochezi dhidi ya  vyombo vya usalama .

Inadaiwa kuwa Mchungaji Msigwa  alikuwa na kibali cha siku tatu cha kufanya mikutano katika jimbo lake na mkutano wa jana ulikuwa wa kwanza.

Marto amesema mikutano yake imefungiwa na hapaswi kuendelea na ziara yake katika kata nyingine mpaka hapo OCD atakapoamua au vinginevyo.

Leo mbunge Peter Msigwa anatakiwa kuripoti kwa RCO na huenda kesi ya uchochezi ambayo tayari imeshafunguliwa jalada lake ikapelekwa Mahakamani .

Imebainishwa kwamba mbunge huyo atazungumza na vyombo vya habari leo mchana kuweka wazi madhila yaliyompata wakati akitekeleza wajibu wake kwa wananchi.

0 Comments:

Post a Comment