Tuesday, November 27, 2012

VIONGOZI WILAYA YA LUDEWA WATAKIWA KUSIMAMIA MAPATO

Viongozi na Watendaji Katika Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa Hususani Mkurugenzi na Mkuu wa Wilaya Wakiwemo Wakuu wa Idara Mbalimbali Wametakiwa Kusimamia Mapato Kikamilifu ILi Kuiongozea Halmashauri ya Wilaya Hiyo Mapato ya Kutosha

Maagizo Hayo Yametolewa na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Kapteni Mstaafu Aseri Msangi Baada ya Kupokea Taarifa ya Wilaya ya Ludewa Alipowasili Wilayani Hapa Kwa Ziara ya Siku Tatu Ambayo Imelenga Maeneo ya Kata Zote za Tarafa ya Mwambao

 Mkuu Huyo Wa Mkoa Alifikia Hatua Hiyo Baada ya Kubaini Wilaya Hiyo Kudumaa na Kukosa Mabadiliko Katika Nyanja Mbalimbali Ikiwemo Kilimo, Uvuvi na Biashara

Kwa Mujibu wa Ratiba, Leo Mkuu wa Mkoa Ataweka Jiwe la Msingi Katika Ofisi ya Kata ya Makonde na Kufanya Mikutano ya Hadhara Katika Kijiji cha Makonde na Lisuma. Kesho Novemba 28 Mkuu wa Mkoa Ataweka Jiwe la Msingi Katika Ujenzi wa Nyumba ya Mganga Kata ya Kilondo na Kufanya Mkuktano wa Hadhara na Kisha Kuweka Jiwe la Msingi Ofisi ya Kata ya Lundila na Kufuatiwa na Mkutano wa Hadhara

 Hata Hivyo Mkuu Huyo wa Mkoa Amewaagiza Wakuu wa Idara Hao Kusimamia na Kufuatilia na Kuacha Kukaa Maofini Badala Yake Waende Vijijini Kuwahimiza Wananchi Katika Shughuli za Maendeleo Mkuu wa Mkoa Anategemea Kumaliza Ziara Yake Novemba 29 Mwaka Huu Ambapo Atapitia Mkoani Mbeya, Kyela, Matema na Kisha Kurudi Mkoani Njombe.

0 Comments:

Post a Comment