Friday, November 30, 2012

SERIKALI YATAKIWA KUONGEZA BAJETI YA MAHAKAMA

 Serikali Imetakiwa  Kuongeza  Bajeti Katika Idara ya Mahakama  Hapa Nchini Ili Kuepuka  Vitendo Vya Rushwa Kwa  Wananchi  Waendeshaji  Mahakama.

Akizungunza na Kituo  Hiki Mwanasheria John Owegi  Ambaye ni Wakili wa Kujitegemea Mkoani Njombe Anesema Ufinyu Wa Bajeti  Katika Mahakama Unapelekea Kuwepo Kwa Mianya ya Rushwa na Kukosesha Haki Kwa  Mtuhumiwa Hali Inayo Pelekea Kupindishwa Kwa Sheria Miongoni Mwa Jamii.

Bwana Owegi Amesema Kuwa Hali Hiyo Inapelekea Kuvunjika Kwa Amani Hapa Nchini  Kutokana na Baadhi ya  Mahakama  Kutotenda Haki Katika Maamuzi ya Kazi na Hivyo Kuleta  Mpasuko  wa Kisheria Kwa Wananchi.

Aidha Amewataka Wananchi Kuwatumia  Mawakili Wa Kujitegemea Katika  Kazi Zao Kutokana  na Mahakama  Kushindwa  Kutenda Haki  Katika Maamuzi  Hali Inayopelekea Kuhukumiwa Kwa Mtu Ambaye  Wakati Mwingine Hana Hatia.

Akijibu Swali Lililouliza Juu ya  Utaratibu Wa  Kutumia Wakilia wa Kujitegemea  Wakili Owegi Amewataka Wananchi Kuondoa  Hofu Juu ya Huduma Zao Kwani Wakati Mwingine Wao Hutoa Huduna ya Kisheria Bure  Kulingana  na Ukubwa wa Kasi  na Kwamba Wao Wapo Kwaajili ya Jamii Hivyo Kinachopelekea  Kumchaji mteja ni  kutokana na wao kulipia leseni.

0 Comments:

Post a Comment