Serikali Imetakiwa Kuongeza Bajeti Katika Idara ya Mahakama Hapa Nchini Ili Kuepuka Vitendo Vya Rushwa Kwa Wananchi Waendeshaji Mahakama.
Akizungunza na Kituo Hiki Mwanasheria John Owegi Ambaye ni Wakili wa Kujitegemea Mkoani Njombe Anesema Ufinyu Wa Bajeti Katika Mahakama Unapelekea Kuwepo Kwa Mianya ya Rushwa na Kukosesha Haki Kwa Mtuhumiwa Hali Inayo Pelekea Kupindishwa Kwa Sheria Miongoni Mwa Jamii.
Bwana Owegi Amesema Kuwa Hali Hiyo Inapelekea Kuvunjika Kwa Amani Hapa Nchini Kutokana na Baadhi ya Mahakama Kutotenda Haki Katika Maamuzi ya Kazi na Hivyo Kuleta Mpasuko wa Kisheria Kwa Wananchi.
Aidha Amewataka Wananchi Kuwatumia Mawakili Wa Kujitegemea Katika Kazi Zao Kutokana na Mahakama Kushindwa Kutenda Haki Katika Maamuzi Hali Inayopelekea Kuhukumiwa Kwa Mtu Ambaye Wakati Mwingine Hana Hatia.
Akijibu Swali Lililouliza Juu ya Utaratibu Wa Kutumia Wakilia wa Kujitegemea Wakili Owegi Amewataka Wananchi Kuondoa Hofu Juu ya Huduma Zao Kwani Wakati Mwingine Wao Hutoa Huduna ya Kisheria Bure Kulingana na Ukubwa wa Kasi na Kwamba Wao Wapo Kwaajili ya Jamii Hivyo Kinachopelekea Kumchaji mteja ni kutokana na wao kulipia leseni.
Friday, November 30, 2012
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Comments:
Post a Comment